Wednesday, July 24, 2013

UCHAKACHUAJI SIO MWENYE MAFUTA TU BALI HATA KATIKA MCHAKATO WA MAONI YA KATIBA MPYA LAKINI....WAZUA ISHU.

https://encrypted-tbn2.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcTjq2GC2dha742SCOV1abaImO4rkhzQrcMVXWDZz5uQMG-k5nDi
KATIBU MKUU WA CCM ABDULRAHMAN KINANA.

WARAKA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa wanachama wake kushinikiza watetea matakwa ya chama hicho kwenye maoni yao katika mchakato wa Katiba Mpya umezua balaa, baada ya Mjumbe wa Tume ya Katiba kumzuia mmoja wa wajumbe wa Mabaraza ya Wilaya kutumia waraka huo kutoa maoni yake.
Alhaj Siad Elmamri ambaye kitaalamu ni mwanasheria, alimzuia Hussein Kiswil aliyekuwa akichangia mapendekezo kwenye rasimu hiyo, baada ya kubaini kuwa, alichokuwa anazungumza kilitokana na maelekezo ya CCM.
Hata hivyo hatua hiyo ilizua tafrani katika mkutano huo, baada ya mjumbe huyo wa baraza la Katiba wilaya, kutoridhika na msimamo huo wa mjumbe wa tume na kupend
ekeza afukuzwe kwenye mchakato huo, kwa kile alichoeleza kuwa anapingana na maelekezo ya kuwaacha watu watoe maoni yao kwa uhuru.
Kiswil alidai kuwa mjumbe huyo hastahili kuendelea na kazi ya kusimamia mabaraza hayo kwa kuwa yeye pamoja na wajumbe wenzake kadhaa, hawana imani naye.
“Siku ya jana (juzi) tukiwa ndani ya ukumbi huu mlitueleza kuwa kila mtu anayo haki ya kutoa maoni yake katika kuchangia Rasimu ya Katiba hii, mimi nilichaguliwa kuingia katika kundi na kupewa jukumu la kuchambua muundo Muungano” alisema Kiswil na kuongeza;
“Nilipoanza kuchangia mimi aliingia Mjumbe wa tume Elmamri na kusikiliza, nilipomaliza kabla hata ya kuruhusiwa na mwenyekiti alianza kuzungumza akisema maoni niliyotoa mimi ni maelekezo ya Chama Cha Mapinduzi na aliongeza kuwa ana taarifa za kuwapo kwa kiongozi mkubwa wa kisiasa aliyekuja Iringa kutoa semina… nilitaka anithibitishie kama hayo aliyoyasema ni ya kweli.”
Alisema kufuatia hatua hiyo ya mjumbe kushindwa kuthibitisha juu ya kuwapo kwa maelezo hayo kutoka CCM na suala la ujio wa kiongozi mkubwa wa CCM  ngazi ya Taifa kuja kutoa semina alipendekeza kikao hicho cha Baraza la Katiba kujadili hoja hiyo aliyotoa na kutolea maamuzi.
Akizungumza mara baada ya kupatiwa nafasi na mwenyekiti wa kikao hicho Omary Shahe Mussa, Elmamri alikiri kutoa ushauri kwa wajumbe kutumia nafasi hiyo kuchangia maoni yao badala ya maoni na msimamo wa chama.
Alisema alitoa ushauri huo kufuatia kusoma kwake habari kutoka katika gazeti la Mwananchi iliyoelekeza maoni na msimamo wa Chama Cha Mapinduzi katika rasimu hiyo na kufafanua kuwa hata mjumbe alitoa yale yaliyokuwa yameshaandikwa na gazeti hili.
“Mwenyekiti waTume Jaji Mstaafu Joseph Warioba alionya juu ya wanasisa kuacha wananchi kutoa maoni yao na alisisitiza kuwa vyama vya kuchangia maoni yao binafsi na si kutoka kwa viongozi wa vyama na kuongeza kuwa alifanya hivyo kutokana na msimamo uliokwishatolewa na Mwenyekiti wa tume hiyo Jaji Mstaafu Joseph Warioba.
Wiki iliyopita, gazeti hili liliripoti habari za CCM kusambaza waraka kwa wanachama wake ambao ni Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ngazi ya wilaya, kutaka wakisaidie chama hicho katika kutetea hoja zake kwenye mchakato wa Katiba Mpya.
Pamoja na mambo mengine, chama hicho kimetofautiana na Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuhusu Muundo wa Muungano, baada ya kupendekeza Muungano wa Serikali mbili badala ya serikali tatu. MWANANCHI.

No comments: