Juma Mtanda, Morogoro.
Timu ya soka ya Kinglwira FC imeishushia mvua ya mabao Kihonda Star katika muendelezo wa ligi daraja la nne msimu wa mwaka 2015/2016 kwa kuicharaza bao 3-0 katika mchezo mkali uliofanyika jana kwenye uwanja wa Sabasaba mkoani Morogoro.
Mshambuliaji wa Kinglwira FC, Nurdin Nurdin ndiye aliyeonekana mwiba mchungu kwa timu ya Kihonda Star kwa kufunga bao mbili pekee katika dakika ya 82 na 90 kufuatia pasi za mwisho za wachezaji Mohamed Mnyepe na Salum Nzange.
Nurdin alifunga mabao hayo moja akifunga kwa tiktaka baada ya mpira wa kona ulioanzishwa na Omari Godfrey kisha kukumiminwa krosi iliyomkuta mfungaji kabla ya kupokea pasi ya Salum Nzange.
Bao la kwanza la Kinglwira lilifungwa na Mohamed Mnyepe dakika ya 43 huku Kihonda Star ikishindwa kufurukuta mbele ya wapinzani wao katika mchezo huo.
Katika michezo mingine timu ya Moro Youth FC ilitembeza kipigo kwa timu ya G-Seven baada ya kuisambaratisha kwa bao 4-1 wakati Don Bosco FC na Uluguay ya Sultan zikishindwa kutambiana baada ya sare ya bao 1-1.
Timu ya Maskan FC yenyewe ilikubali kutandikwa bao 1-0 mbele ya Barafu FC ya Kihonda na Magadu FC na Lubungo FC zilishindwa kucheza mchezo wao Desemba 26 ikipisha ligi daraja la kwanza kwa mchezo baina ya Polisi Moro SC na Burkina katika mchezo uloisha kwa sare ya bao 2-2.
Katika mchezo huo kati ya Magadu FC na Lubungo FC utachezwa januari mosi ambapo katika mchezo wa leo (jana) Moro City FC itaonyesha umwamba na Chipolopolo FC saa 10 jioni katika uwanja wa Sabasaba.CHANZO:MTANDA BLOG
Wednesday, December 30, 2015
KUTOKA KWENYE MAGAZETI YA HARDNEWS JUMATANO DECEMBA 30/ 2015 YAKIWA NA VICHWA VIKUU VYA HABARI

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.

.
Friday, August 21, 2015
EDWARD LOWASSA, DKT JUMA DUNI HAJI WARUDISHA FOMU TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI LEO JIJINI DAR ES SALAAM
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Damian Lubuva akimkabidhi, Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, nyaraka mbalimbali zitakazotumika wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu, kwenye Ofisi za Tume hiyo, Jijini Dar es salaam leo Agosti 21, 2015. Kushoto ni Mgombea Mweza wake, Dkt. Juma Haji Duni.CHANZO OTHMANI MICHUZI
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Damian Lubuva akizungumza mara baada ya kupokea Fomu zilizorudishwa na Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa na Mgombea Mweza wake, Dkt. Juma Haji Duni baada ya kukamilisha mchakato wa kutafuta wadhamini katika Mikoa 10 ya Tanzania na kutimiza masharti yote ya Uchaguzi, leo Agosti 21, 2015 kwenye Ofisi za Tume hiyo, Jijini Dar es salaam.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutangazwa rasmi na Tume ya Uchaguzi kuwania nafasi hiyo, leo Agosti 21, 2015 kwenye Ofisi za Tume hiyo, Jijini Dar es salaam. Pembeni yake ni Mgombea Mweza wake, Dkt. Juma Haji Duni
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, Mgombea Mweza wake, Dkt. Juma Haji Duni pamoja na viongozi wengine waliowasindikiza, wakitoka kwenye ofisi za Tume ya Uchaguzi baada ya kurudisha fomu leo Agosti 21, 2015.
Subscribe to:
Comments (Atom)






